
MBEYA CITY;
Imekuwa na mwanzo mzuri katika Ligi Kuu, ikipanda msimu huu na kufanikiwa kuwa moja ya timu zilizo katika mbio za taji. City ingeweza kumaliza mzunguko wa kwanza kileleni kama isingeruhusu kusawazishiwa bao na Azam FC na kutoa sare ya 3-3 katika mechi ya mwisho. Bado ina nafasi ya kuvunja rekodi ya Tukuyu Stars ya Mbeya pia, iliyopanda Ligi Kuu na moja kwa moja kuchukua taji mwaka 1986. Katika mechi 13, imeshinda saba, sare sita, haijafungwa, imefunga mabao 19, imefungwa 10 na imemaliza na pointi 27.
P W D L GF GA GD Pts
0 comments:
Post a Comment