AZAM FC;
Haikuwa na mwanzo mzuri sana, lakini baadaye ikasimama imara na kupanda kileleni kabla ya kuja kuenguliwa na Yanga SC siku ya mwisho ya mzunguko wa kwanza. Pamoja na hayo, Azam bado ni timu imara na inaweza kutimiza ndoto zake za kutwaa taji la kwanza la ubingwa wa Bara msimu huu, licha ya kumpoteza kocha wake, Muingereza, Stewart Hall aliyejiuzulu siku ya mwisho. Katika mechi 13, imeshinda saba, sare sita, haijafungwa hata moja, imefunga mabao 23, imefungwa 10 na imemaliza na pointi 27.
P W D L GF GA GD Pts
2 Azam 13 7 6 0 23 10 13 27
0 comments:
Post a Comment