Meneja
mpya wa klabu ya Man utd Louis van Gaal ametangaza msisitizo wa kutaka
wachezaji watatu kusajiliwa na mashetani wekundu kabla ya kuanza kwa
ligi kuu ya soka nchini Uingereza August 16 mwaka huu.
Van
Gaal, ambaye anatarajiwa kuwasili mjini Manchester juma hili ametoa
agizo kwa viongozi wa klabu ya Man Utd kuhakikisha washambuliaji Arturo
Vidal, Angel Di Maria pamoja na beki Mats Hummels wanasajiliwa haraka
iwezekanavyo.
Meneja
huyo kutoka nchini Uholanzi amesema anaamini hakuna linaloshindikana
katika harakati za kuwasajili wachezaji hao watatu hivyo suala la
kuwapata lipo mikononi mwa viogoni kwa kushirikiana na benchi la ufundi
ambalo litakuwa chini yake.
Tayari
mshambuliaji kutoka nchini Argnetina na klabu ya Real Madrid Angel Di
Maria ameshaweka wazi dhamira ya kutaka kucheza soka katika ligi ya
nchini Uingereza, ili hali mshambuliaji kutoka nchini Chile pamoja na
klabu bingwa nchini Italia Juventus, Arturo Vidal yupo tayari kuondoka
mjini Turine.
Kwa
upande wa Hummels anayeitumikia klabu ya Borussia Dortmund, bado
haijathibitika kama yu radhi kuondoka nchini Ujerumani kwa sasa.
0 comments:
Post a Comment