SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Mshambuliaji huyu ambaye alikuwa tegemeo Mtibwa Sugar kabla ya msimu wa 2010 kusajiliwa na Yanga na kuiwezesha kutwaa Kombe la Kagame mwaka 2011 na pia kuibuka mfungaji bora, baada ya hapo amepotea. 
YANGA imeonekana kuwa ni timu yenye nuksi kwa wachezaji wanaotoka Mtibwa Sugar kwani wote waliohamia hapo Jangwani wakitokea Manungu, kwa sasa wanasugua benchi.
Kwa misimu mitatu mfululizo sasa, Yanga imesajili wachezaji kutoka Mtibwa. Waliotua hapo ni Said Bahanuzi, Juma Abdul, Hussein Javu na Rajab Zahir.
Ingawa kipa, Deogratius Dida, naye aliwahi kuidakika Mtibwa Sugar siku za nyuma, lakini alisajiliwa Yanga akitokea Azam FC.  Abdul na Bahanuzi wako muda mrefu ndani ya timu hiyo ingawa hawapati namba kutokana na nafasi zao kuwa na wachezaji wengine ambao hawakamatiki. Zahir na Javu ambao walikuwa tegemeo wakiwa Mtibwa Sugar,  wamesajili Yanga msimu huu. Hata hivyo nao wamekosa namba za kudumu na mara nyingi huishia benchi.
Said  Bahanuzi
Mshambuliaji huyu ambaye alikuwa tegemeo Mtibwa Sugar kabla ya msimu wa 2010 kusajiliwa na Yanga na kuiwezesha kutwaa Kombe la Kagame mwaka 2011 na pia kuibuka mfungaji bora, baada ya hapo amepotea. Alianza kuishia kukaa benchi lakini siku hizi hata jezi havai anaishia jukwaani.
“Mimi naamini nina kipaji na najua mpira, lakini kuwa majeruhi mara kwa mara kumechangia kupoteza mwelekeo wa soka langu, bado napambana na naamini ipo siku  nitacheza tu na kurudi kama zamani, hakuna mtu ambaye hapendi kuanza kikosi cha kwanza, ila uamuzi wote ya nani acheze unabaki kwa kocha,” alisema Bahanuzi.
Juma Abdul
Beki wa kulia wa kutegemewa wa zamani ya Mtibwa. Alitua Yanga mwaka 2011, lakini alicheza kidogo kikosi cha kwanza ndani ya timu hiyo kabla ya kupotezwa na ujio wa Mbuyu Twite anayeishikilia nafasi hiyo.
Beki huyo, ambaye anasifika kwa mipira ya krosi, amekuwa akipata nafasi ndani ya timu wakati baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wakiwa majeruhi au wanapotumikia adhabu. Pia amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kuwa majeruhi mara kwa mara, hata sasa anasumbuliwa na uvimbe kwenye vidole vya mguuni. “Uwezo wa kucheza kikosi cha kwanza ninao, lakini timu ina wachezaji wengi na kila mmoja anataka kucheza hivyo kocha ndio anaamua nani aanze kikosi cha kwanza na nani aanzie benchi ila uwemo mimi ninao mkubwa tu,” anakiri.
Hussein Javu
Alipokuwa Mtibwa msimu uliopita aliyewazamisha Yanga katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Mtibwa ilishinda mabao 3-0 wakati yeye akifunga mawili.
Wengi walidhani angeanza kikosi cha kwanza kwa kiwango alichokionyesha Mtibwa, lakini kwa ushindani wa namba kwenye nafasi ya ushambuliaji uliopo Yanga, amejikuta benchi likiwa ndio anga zake.

“Nafurahi kuwa Yanga kwani ni timu kubwa ingawa bado sijapata nafasi ya kucheza mara kwa mara.
Lakini naamini muda wangu ukifika nitacheza, kama unavyoona hapa kuna ushindani mkubwa wa namba katika nafasi ninayocheza, ni tofauti na ilivyokuwa Mtibwa,” alisema Javu.
Rajab Zahiri
Amesajiliwa Yanga msimu huu katika nafasi ya beki wa kati, lakini amejikuta akiishia benchi mara kwa mara kwani hawezi kuwaondoa Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani.
Hucheza mara moja moja kama baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wakiwa wagonjwa, lakini zaidi ya hapo kukaa benchi ni kawaida yake.
Kocha wake, Ernest Brandts, alifanya uamuzi mgumu wa kumweka nje Cannavaro katika mchezo dhidi ya Mgambo JKT wiki mbili zilizopita na kumchezesha kinda huyu, hata hivyo alivurunda na  akatolewa kipindi cha pili, uwezekano wa kupangwa tena ni finyu.
“Sina tatizo na kocha (Ernest Brandts). Kinachonisumbua ni suala la kuwa majeruhi. Yaani nikipona hili, naumwa hili tangu nifike hapa  hivyo bado sijawa fiti sana,” anasema Zahir.
Categories:

0 comments:

Post a Comment

    Blogger news

    Blogroll

    Pages

    About